Pages

Friday, March 23, 2012

Maonyesho ya Harusi Yarudi Tena Kwa Kishindo



Marketing Manager for Harusi Trade Fair  explaining to the press concerning Harusi Trade Fair 2012 at Maelezo Posta Dar-es-salaan on 23rd-March-2012
--
Kwa awamu ya tatu  maandalizi ya maonyesho ya Harusi yanayotarajia kufanyika tarehe 30 machi hadi 1 april katika ukumbi wa Diamond Jubilee  yatakua na washiriki na wadau mbalimbali waliobobea kwenye maswala ya Harusi pamoja na mahitaji yote ya Harusi.



 Muanzilishi na muandaaji wa maonyeshao haya ya kila mwaka Mustafa Hassanali  alisema“ Maonyesho ya mwaka huu yatakua makubwa sana kulinganisha na ya mwaka jana na tunatazamia kuyafanya maonyesho haya ya Harusi kuwa maonyesho makubwa nchini kote miaka ijayo”.



Ukweli katika nukuu, Maonyesho haya ya Harusi yalowavutia zaidi ya wafanya maonyesho 40  waliothibitisha ushiriki wao,wengi wakiwa waliwahi kushiriki katika miaka iliyopita ,wameweza kuona ukuaji katika maonyesho haya..



“ Harusi inaleta umoja katika familia na jamii na ni moja kati ya nyakati pekee zinazotokea katika maisha,hivyo mpango wetu ni kutoa mahitaji ya bibi Harusi na bwana Harusi katika sehemu moja na huu ni wakati muafaka wa wao kujipatia uzoefu katika bidhaa na huduma zote harusi,” alisema meneja masoko Hamis K Omary.



Maonyesho ya Harusi  yanaleta pamoja  wadau na wachuuzi  mbalimbali waliobobea katika maswala ya Harusi na kufanya  maonyesho haya kuwa na kiwango na uhakika nchini Tanzania. Kati ya  wachuuzi mbalimbali watakaoshiriki mwaka huu ni wachuuzi  wa keki, maua, wapiga picha, gauni za harusi, tovuti za wabunifu wa harusi, pamoja  ubunifu mbalimbali unaousiana na maswala mazima ya harusi.



 Mmoja kati ya washiriki katika maonyesho y Harusi 2012, ni Gabriel Makupa wa GRM productions, ambae  ni mtayarishaji  maarufu wa picha mbalimbali za Harusi. “ Tumepata uzoefu mzuri kwa mwaka ulopita ulotusaidia kupata wateja na nafasi ya kukuza  biashara. Tulitangaza bidhaa na huduma zetu na kukuza idadi ya wateja kwenye maonyesho ya Harusi 2010 na ndio maana tunashiriki kuanzia kipindi hicho.



Kuna nafasi chache tu ambazo zinapatikana katika maonyesho ya mwaka huu.“Mpaka sasa makampuni 40 yanayohusika na maswala mbalimbali ya Harusi yamedhibitisha ushiriki wao na tunatarajia idaidi ya washiriki kuongezeka.So far 40 wedding related. Mwaka huu tuna bidhaa mpya kabisa kwa wafanyabiashara wadogo wadogo ili na wao waweza kukua.kwa hivyo tunawaomba wale wote wanaohusika na maswala ya Harusi kushiriki katika maonyesho haya ya Harusi” alimalizia Bw. Omary
 
Ikiwa ni msimu wa Harusi katika  kipindi hiki cha pasaka, maonyesho  haya ya Harusi si yakukosa kwa familia, marafiki,na wanakamati wa Harusi.huu ni wakati wa kupata vipaji vya ubunifu katika mambo yote ya Harusi.



Maonyesho ya Harusi 2012 ni bure kwa watu wote kuhudhuria



Maonyesho ya Harusi 2012 yamedhaminiwa  Clouds FM, Clouds TV, The Citizen, Global Outdoor Systems, 2M Media, Ultimate Security, Vayle Springs, Eventlites, MH Gallery, Dar411, Epidor na 361 degrees.

0 comments: